Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, Mehol Sadai Mkuu wa Tume ya Kitaifa ya Waislamu Ufilipino Jumapili Agosti 5 amewatumia barua wakuu wa Chuo cha Pilar katika eneo la Zamboanga lenya idadi kubwa ya Waislamu akitaka uamuzi huo ubatilishwe.
Baraza la mji wa Zamboanga limekitaka chuo hicho kitafkari upya uamuzi huo. Inaaminika kuwa chuo hicho cha kikatoliki ndio cha kwanza kupiga marufuku Hijabu nchini Ufilipino.
Sadain amesema kuwa sera za kielimu nchini humo zinabainisha wazi kuwa wanafunzi Waislamu wa kike wana haki ya kuvaa Hijabu wakiwa katika shule na vyuo vya elimu na kwamba hawapaswi kulazimishwa kushiriki katika hafla zinazokinzana na Uislamu.
Karibu asilimia 80 ya watu milioni 100 Ufilipino ni Wakatoliki huku aghalabu ya waliosaliwa wakiwa ni Waislamu waishio kusini mwa nchi hiyo ya Asia.
1071625