IQNA

Iran yashangazwa na kimya cha taasisi za kimataifa kuhusu mauaji ya Myanmar

17:22 - August 08, 2012
Habari ID: 2388712
Mbunge mmoja wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameshangazwa na kimya cha Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) kuhusiana na jinai zinazotekelezwa na makundi ya kigaidi nchini Syria na vilevile mauaji ya kinyama yanayofanywa na serikali ya Myanmar dhidi ya Waislamu wa Rohingya nchini humo.
Kwa mujibu wa Press TV, matamshi hayo yametolewa na Ali Iranpur mbunge wa eneo bunge la Mubarakeh katika bunge la Iran na kuongeza kuwa, kimya cha taasisi hizo kuhusu matukio ya nchi hizo ni jambo lisilokubalika kabisa. Amesema nchi za Magharibi zinaingilia masuala ya Syria kwa lengo la kugawa na kuwagonganisha Waislamu wa nchi hiyo.
Kuhusiana na suala la Myanmar ripoti za hivi karibuni zinabaini kwamba zaidi ya Waislamu 650 wameuawa kinyama na askari usalama pamoja na wanamgambo wanaungwa mkono na serikali na pia kupelekea maelfu ya wengine kukimbia makazi yao kutokana na woga wa kuuliwa na magaidi wa Kibudha.
Serikali ya Myanmar imekataa rasmi kutambua haki za kimsingi za Waislamu wa nchi hiyo kwa hoja kuwa asili yao ni ya nchi nyingine. Hii ni katika hali ambayo historia ya nchi hiyo inapinga madai hayo yasiyo na msingi na kuthibitisha kwamba Waislamu waliingia nchini humo katika karne ya nane. 1074053
captcha