IQNA

Mgomo wa kuketi chini wa kutetea makaburi ya Baqii wafanyika Iraq

15:57 - August 29, 2012
Habari ID: 2400977
Mgomo wa kuketi chini kwa ajili ya kutetea makaburi ya Baqii katika mji mtakatifu wa Madina sambamba na kuwadia mwaka wa 89 tangu watawala wa Saudi Arabia wavunje makaburi hayo ya Ahlul Bait wa Mtume (saw) na masahaba wake umefanyika leo katika mpaka wa Iraq na Saudi Arabia.
Wafanyamgomo hao wametaka kujengwa upya makaburi ya Maimamu na masahaba wa Mtume (saw) na kutovunjiwa heshima eneo hilo linalozuriwa na Waislamu.
Raia hao wa Iraq pia wamesisitiza juu ya udharura wa Mawahabi kuacha kuvunjia heshima matukufu ya Kiislamu.
Mgomo huo umewashirikisha wanaharakati wa kidini, maulamaa na matabaka mbalimbali ya wananchi wa Iraq.1087042

captcha