Mkutano huo unaofanyika chini ya kaulimbiu ya "Vyombo vya habari vya muqawama, mwamko wa Kiislamu hadi Kufikia Ushindi" unahudhuriwa na wawakilishi wa vyombo vya habari zaidi ya 280 kutoka nchi 35 katika mabara matano ya dunia.
Katika hafla ya ufunguzi wa mkutano huo, Hujjatul Islam wal Muslimin Ali Karimiyan Katibu Mkuu wa Umoja wa Redio na Televisheni za Kiislamu amewasilisha ripoti kuhusu shughuli za Baraza Kuu la jumuiya hiyo.
Naye Ali Larijani Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran ambaye alikuwa mgeni rasmi na mzungumzaji mkuu katika mkutano huo ameeleza mitazamo yake kuhusu Mkutano wa Sita wa Baraza Kuu la Umoja wa Redio na Televisheni za Kiislamu ulioanza leo hapa Tehran.
Moja kati ya ratiba za mkutano wa leo alasiri ilijumuisha uonyeshaji wa athari za tamasha zilizochaguliwa pamoja na filamu fupi fupi kuhusiana na mwamko wa Kiislamu. 1105064