Kwa mujibu wa tovuti ya Biladi, serikali ya Morocco imepiga marufuku kwa muda wa wiki moja uuzaji wa majarida sita ya Hispania na Ufaransa pamoja na gazeti moja la Ujerumani.
Akizungumzia suala hilo, Mustafa al-Khalafi, Waziri wa Habari na Mawasiliano wa Morocco amesema kwamba wananchi wa nchi hiyo wamefurahia sana uamuzi huo wa serikali.
Wachambuzi wa mambo wanaamini kwamba majarida mawili ya Hispania na Ufaransa yalichapisha vikatuni vya kumvunjia heshima Mtume (saw) ili kunufaika kifedha, kutokana na matatizo makubwa ya kiuchumi yanazozikumba nchi za Ulaya. 1112508