Kituo cha Palestine Info kimeandika kuwa, gazeti la Kizayuni la Maariv limeripoti kuwa watumiaji wengi wa Kiisraeli wa simu ya Iphone 5 wanalalamika sana kutokana na kwamba ramani za simu mpya ya kampuni ya Apple haiutambui mji wa baitul Muqaddas kuwa ni mji mkuu wa Israel.
Gazeti hilo limeandika kuwa, watumiaji wa Iphone 5 wamegundua kwamba program za simu hiyo haziutambulishi mji wa Baitul Muqaddas (Jerusalem) kuwa ni mji mkuu wa Israel japokuwa simu hiyo imezitaja nchi ngingine pamoja na miji mikuu yao.
Gazeti la Kizayuni la Maariv limeongeza kuwa program ya simu mpya ya Apple imeweka program mpya ya ramani badala ile ya Gogle Map na kuweka alama ya nyota katika miji mikuu ya nchi mbalimbali lakini haikuweka mji mkuu kwa ajili ya Israel.
Vilevile program ya wakati wa kimataifa ya simu ya Iphone 5 haiutambui mji wa Baitul Muqaddas kuwa ni mji mkuu wa Israel. 1115454