Amesisitiza kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel hauna budi ila kukubali haki za kisheria za Wapalestina.
Akizungumza mjini Beirut Jumamosi usiku, Nasrullah amesema Rais Barack Obama wa Marekani anaweza kusitisha hujuma za Israel huko Ghaza kwa kupiga simu mara moja tu lakini hafanyi hivyo. Kiongozi wa Hizbullah ameipongeza harakati ya Hamas kwa kufanikiwa kuvurumisha makombora katika mji wa Tel Aviv na ameuonya utawala wa Kizayuni kutothubutu kutekelelza hujuma ya nchi kavu dhidi ya Ghaza. Sayyid Hassan Nasrullah pia amezikosoa vikali nchi za Kiarabu na Kiislamu kwa kushindwa kuchukua hatua za kivitendo kwa ajili ya kukomesha hujuma za Israel huko Ghaza.
1139227