IQNA

Wazayuni watofautiana na Netanyahu kuhusu Iran

14:33 - January 15, 2013
Habari ID: 2480767
Uchunguzi wa maoni uliofanywa na gazeti la The Times la utawala haramu wa Israel unaonyesha kuwa idadi kubwa ya Wazayuni hawatilii maanani porojo za kila siku za Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kwamba Iran inakaribia kumiliki silaha za nyuklia.
Uchunguzi huo umeonyesha kwamba, asilimia 43 ya Wazayuni wanatiwa wasiwasi na hali mbaya ya kiuchumi na ukosefu wa ajiri kwa vijana wa Israel. Netanyahu amejaribu kufunika ukweli huo kwa kuwahadaa Wazayuni kwamba tishio kubwa linalowakabili ni Iran na kwamba miradi ya kuzalisha nishati ya nyuklia ya Tehran ina malengo ya kijeshi.

Duru za habari zinaripoti kwamba, washauri wa Benjamin Netanyahu wamemtaka abadili stratejia yake na kuangazia changamoto zinazoukabili utawala huo ghasibu badala ya kupiga domo kuhusu Iran iwapo anataka kupata ushindi kwenye uchaguzi wa wiki ijayo.

1171485
captcha