Kwa mujibu wa ripota wa Shirika la Habari la Kimataifa la Qurani (Iqna) limeandika kuwa, Nargese Bibimoune binti wa Kiislamu anayeishi katika mji wa Lyon nchini Ufaransa, amepigwa marufuku wakati alipokuwa akitaka kujiandikisha kwenye somo la michezo kwenye klabu moja iliyoko katika kitongoji cha Givors. Hii si mara ya kwanza kwa jamii ya wanawake wa Kiislamu nchini humo kukabiliwa na vitendo vya kibaguzi vinavyotekelezwa kwa misingi ya kidini. Inafaa kuashiria hapa kuwa, Waislamu wamepigwa marufuku kuingia kwenye klabu moja ya michezo iliyoko katika eneo la Vigneux- sur-Seine kusini mwa jiji la Paris.
1206135