Akizungumza katika mahojiano maalumu na kanali ya televisheni ya al-Mayadeen yenye makao yake Beirut Jumatano usiku, Katibu Mkuu wa Hizbullah Sayyed Hassan Nasrullah amesema Hizbullah haitauruhusu utawala haramu wa Israel ukiuke ardhi ya Lebanon.
Ikumbukwe kuwa mnamo Agosti 7 milipuko miwili iliwajeruhi wanajeshi vamizi wa Israel ambao walikuwa wameingia mita 400 ndani ya ardhi ya Lebanon katika eneo la kusini. Sayyed Nasrallah amesema, ‘Hizbullah ilikuwa na taarifa za mapema kuwa wanajeshi wa Israel walikuwa wamepanga kuingia kusini mwa Lebanon na hivyo harakati hiyo ilitega mabomu ambayo yalilipuliwa kutokea mbali wakati wanajeshi hao wa Israel walipofika hapo.’
Kufuatia milipuko hiyo jeshi la Lebanon lilitoa taarifa na kusema uingiaji huo wa askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel ni ‘ukiukaji wa mamlaka ya Lebanon’.
1272976