Mpango huo ulizinduliwa hivi karibuni na unajumuisha msafara wa Daawa, zahanati za muda, mashindano ya Ramadhani, futari kwa wapita njia, kukarabati misikiti, kuandaa mashindano ya michezo na hatimaye kutoa zawadi za nguo kwa mnasaba wa Siku Kuu ya Idul Fitr kwa familia za wasiojiweza katika nchi hiyo ya Afrika.
Akizungumza na waandishi habari, Waziri wa Usalama wa Jamii Sudan Ibrahim Adam Ibrahim amepongeza mpango huo wa vijana wa Sudan na kusema jamii inahitaji ubunifu kama huo unaowalenga watu wasiojiweza katika jamii. Aidha ametoa wito kwa Wasudani kuendeleza mafundisho ya Kiislamu ya kuwasaidia wasiojiweza. Mwenyekiti wa Muungano wa Vijana wa Sudan Dkt. Shogar Bashar amesema mpango huo utajumuisha majimbo yote ya nchi hiyo na kwamba tayari kuna misafara tayari imeshatumwa katika maeneo mbali mbali. Amesema muungano huo umeshakarabati misikiti zaidi ya 3,000 na kutayarisha vifurushi 80,000 vya chakula kwa ajili ya familia masikini katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.../mh