Miongoni mwa mahujaji takribani 2,000 wakiwemo Wairani 136 waliothibitishwa kupoteza maisha katika maafa ya Mina Alhamisi iliyopita, walikuwemo maqarii wawili wa kimataifa wa Iran, Mohsen Hajihassani Kargar na Amin Bavi.
Maustadhi waandamizi wa Qur'ani Misri Ahmad Ahmad Noaina, na Muhammad Taha Abdul Wahab.
Katika ujumbe wake, Ustadh Noaina ameliitaja tukio la Mina kuwa maafa makubwa na kutuma salamu zake za rambi rambi kwa jamii ya Qur'ani nchini Iran na familia za maqarii hao wawili. Naye Ustadh Abdul Wahab ametuma salamu zake za rambi rambi kufuatia vifo vya maqarii hao wawili.
Ustadhi wa Qur'ani kutoka Iran Adnan al Salehi na qarii wa kimatiafa Yahya al Sahaf pia wametuma salamu za rambi rambi kufuatia vifo vya Hajihassani Kargar and Bavi.../mh