IQNA

Nakala za Qur'ani 5,000 zasambazwa katika Maonyesho ya Kimataifa ya Vitabu Kuwait

14:57 - November 30, 2025
Habari ID: 3481590
IQNA – Wageni wa Maonyesho ya 48 ya Vitabu Kimataifa mjini Kuwait wamepewa zawadi ya nakala zaidi ya 5,000 za Qur'ani Tukufu. Banda la Wizara ya Mambo ya Kiislamu ya Saudi Arabia limesambaza nakala hizo, kwa mujibu wa taarifa ya Al-Madinah.

Banda hilo limepokelewa kwa furaha na wageni, waliotambulishwa nakala za Qur'ani zilizochapishwa kwa ukubwa tofauti, miradi ya Saudi katika uchapishaji na tafsiri ya Qur'ani kwa lugha mbalimbali, pamoja na shughuli za Kiislamu za nchi hiyo. Ushiriki wa Saudia katika tukio hili ni sehemu ya juhudi za taifa kushiriki majukwaa ya kimataifa, kuimarisha mwingiliano na jamii na kueneza Qur'ani duniani.

Maonyesho ya 48 ya Vitabu Kimataifa Kuwait yalifunguliwa Novemba 20, 2025, yakihusisha nyumba za uchapishaji 611 kutoka nchi 33 za Kiarabu na zisizo za Kiarabu. Yalifanyika chini ya kauli mbiu “Mji Mkuu wa Utamaduni; Ardhi ya Vitabu” na kufungwa Jumamosi, Novemba 29.

Mwaka huu maonyesho yameambatana na uteuzi wa Kuwait kama Mji Mkuu wa Utamaduni na Vyombo vya Habari wa Kiarabu kwa mwaka 2025, huku Oman ikiwa mgeni wa heshima.

captcha