IQNA

Wazayuni wauhujumu na kuuvunjia heshima Msikiti wa al Aqsa

11:26 - September 28, 2015
Habari ID: 3372690
Jumapili wanajeshi wa utawala haramu wa Israel waliushambulia na kuuvunjia heshima tena Msitiki wa al Aqsa huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu suala lililozusha mapigano makali baina ya askari hao na Waislamu waliokuwa msikiti hapo wakitekeleza ibada.

Wanajeshi  hao wa utawala wa Kizayuni Israel pia waliwashambulia Waislamu wa Palestina waliokuwa ndani ya msikiti huo kwa risasi na gesi ya kutoa machozi.
Wakati huo huo magenge ya walowezi wa Kiyahudi wenye misimamo ya kufurutu ada waliokuwa wakisaidiwa na wanajeshi wa Israel walishambulia eneo la Babul Silsila katika Msikiti wa al Aqsa kwa lengo la kuchochea Waislamu waliofanya mgomo ndani ya msikiti huo na kukabiliwa na majibu makali ya Wapalestina.
Eneo la Msikiti wa al Aqsa limekuwa uwanja wa mapigano makali baina ya wanajeshi wa Israel na Wapalestina tangu wiki mbili zilizopita kutokana na hujuma ya walowezi wa Kizayuni waliokwenda eneo hilo kwa kutumia visingizio mbalimbali. Makumi ya Wapalestina wamejeruhiwa katika hujuma hizo na wengine wengi wametiwa nguvuni na kupelekwa kusikojulikana na askari wa utawala bandia wa Israel.

3372664

captcha