IQNA

Mwanamasumbwi Muhammad Ali aaga dunia akiwa na miaka 74

22:30 - June 04, 2016
Habari ID: 3470357
Bingwa wa ndondi raia wa Marekani mwenye asili ya Afrika, Muhammad Ali ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 74.
 

Mwanamasumbwi Muhammad Ali aaga dunia akiwa na miaka 74
Bingwa huyo wa zamani wa mchezo wa Masumbwi Dunia kwa uzito wa juu (World Heavyweight Champion) ameaga dunia katika hospitali moja mjini Phoenix jimbo la Arizona, alikolazwa tangu Alkhamisi iliyopita kutokana na matatizo ya kupumua.

Mwanamasumbwi Muhammad Ali aaga dunia akiwa na miaka 74
Imearifiwa kuwa, matatizo hayo ya kupumua yalitokana na ugonjwa wa kutetemeka alioupata tangu mwaka 1984. Msemaji wa familia ya Muhammad Ali amewashukuru wote waliosimama na nyota huyo wa ndondi alipokuwa anaugua hadi wakati wa kifo chake na kusisitiza kuwa kwa sasa familia hiyo inahitaji faragha. Taarifa ya familia ya mwanamasumbwi huyo imesema bingwa huyo mara 3 wa mashindano ya kimataifa ya Olimpiki atazikwa nyumbani kwake mjini Louisville, eneo la Kentucky.

Mwanamasumbwi Muhammad Ali aaga dunia akiwa na miaka 74

Itakumbukwa kuwa, bingwa huyo wa ndondi aliyejiunga na mchezo huo akiwa na umri wa miaka 12, alifahamika kama Cassius Clay, lakini akabadilisha jina na kuitwa Muhammad Ali baada ya kujiunga na dini tukufu ya Kiislamu mwaka 1964.

3503744



captcha