IQNA

Wanajeshi Wairaqi wasoma Qur’ani katika eneo walilokomboa kutoka magaidi wa ISIS

23:39 - July 29, 2016
Habari ID: 3470483
Wanajeshi Wairaqi wamekuwa na kikao maalumu cha kusoma Qur’ani katika huko Saad al A’adhim katika mkoa wa Diyala, eneo ambalo wamelikomboa hivi karibuni kutoka kundi la kigaidi la ISIS au Daesh.

Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, kikao hicho cha Qur’ani kimeandaliwa na Taasisi ya Darul Qur’ani ya Idara ya Usimamizi wa Haram ya Imam Hussein AS.

Idadi kubwa ya wanajeshi, maafisa wa usalama na wapiganaji wa kundi la kujitolea la wananchi lijulikanalo kama Hashd al-Shaabi, walishiriki katika kikao hicho cha kusoma Qur’ani Tukufu.

Maeneo ya Kaskazini na Magharibi mwa Iraq yamekuwa yakishuhudia mapigano na ukatili mbaya sana tokea magaidi wa ISIS wakalie kwa mabavu maeneo hayo kuanzia Juni mwaka 2014.

Katika miezi ya hivi karibuni wanajeshi wa Iraq wakishirikiana na wapiganaji wa kujitokea wamefanikiwa kukomboa maeneo mengi yaliyokuwa yakikaliwa kwa mabavu na ISIS.

Mapema wiki hii, Waziri wa Ulinzi wa Iraq alitangaza kuwa, wapiganaji wa kundi la kigaidi la ISIS wanaendelea kuzidiwa nguvu na vikosi vya ulinzi vya nchi hiyo na wameendelea kuhama ngome zao na kukimbilia katika maeneo mengine.

Khaledal-Obaidi ametangaza kuwa, vikosi vya Iraq vimeendelea kupata mafanikio katika operesheni zake za kuwatimua katika ardhi ya nchi hiyo wapiganaji wa kundi la kigaidi la ISIS.

Wanajeshi Wairaqi wasoma Qur’ani katika eneo walilokomboa kutoka magaidi wa ISISWanajeshi Wairaqi wasoma Qur’ani katika eneo walilokomboa kutoka magaidi wa ISISWanajeshi Wairaqi wasoma Qur’ani katika eneo walilokomboa kutoka magaidi wa ISIS

3518567

captcha