IQNA

Malefu ya Wapalestina washiriki katika Sala ya Ijumaa Msikiti wa Al Aqsa

Malefu ya Wapalestina washiriki katika Sala ya Ijumaa Msikiti wa Al Aqsa

9:08 - February 29, 2020
Habari ID: 3472514
TEHRAN (IQNA) - Maelfu ya Wapalestina walishiriki katika Salatul Fajr katika Msikiti wa Al Aqsa mjini Quds (Jerusalem) Ijumaa asubuhi licha ya vizuizui vikali vilivyokuwa vimewekwa na jeshi la utawala wa Kizyauni wa Israel.

Kwa mujibu wa taarifa maelfu ya Wapalestina walihudhuria Sala ya Ijumaa katika misikiti mingine 200 mjini Quds na maeneo mengine ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.

Kujitokeza kwa wingi waumini kushiriki katika sala ya jamaa jana alfajiri ni kama sehemu ya kampeni  ya Alfajiri Adhimu.

Kamepni hiyo ilianza wiki chache zilizopita kwa lengo la kuuhami Msikiti wa Al Aqsa na maeneo mengine matakaitfu ya Wapalestina ambayo yanakabiliwa na hujuma na jma za Wazayuni..

Katika wiki za hivi karibuni wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wamekuwa wakiwashhambulia Wapalestina wanaoshiriki katika Sala ya Alfajiri na kuwakamata baadhi yao.

3470772

captcha