IQNA

Katibu Mkuu wa UN alaani ubaguzi, chuki dhidi ya Waislamu

20:57 - March 19, 2021
Habari ID: 3473747
TEHRAN (IQNA)- Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amelaani chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu (Islamophobia) na kusema ubaguzi wa rangi kwa bahati mbaya sana upon a unaendelea katika nchi zote na katika jamii zote duniani na mizizi yake imekita kutokana na karne na karne za ukoloni na utumwa.

Gutteres ameyasema hayo katika tukio la kuadhimisha siku ya kimataifa ya kupinga ubaguzi wa rangi iliyofanyika leo kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, asilimia kubwa ikiwa ni kwa njia ya mtandao.

Guterres amesema “Tunauona ubaguzi ulioenea na kutengwa na kuteswa kwa watu wa asili ya Kiafrika. Tunauona katika dhuluma na ukandamizaji unaovumiliwa na watu wa kiasili na makabila mengine madogo. Tunauona katika maoni yenye kuchukiza ya wanaoona wazungu ni bora zaidi na kwenye vikundi vingine vyenye msimamo mkali. Tunaona pia ubaguzi wa rangi na ubaguzi katika chuki dhidi ya Uyahudi, chuki dhidi ya Waislamu, unyanyasaji wa jamii ndogo za Kikristo na aina zingine za kutovumiliana na chuki dhidi ya wageni. Na tumeuona ubaguzi wa rangi katika vurugu za hivi karibuni za kuchukiza dhidi ya watu wa asili ya Asia, wanaolaumiwa bila haki kwa kusambaza COVID-19.”
 Ameongeza kuwa ubaguzi upon a unaendelea kuwepo kwani unashuhudiwa pia katika upendeleo uliojengeka katika kutambua sura na akili bandia.

Katika kusisitiza kuhusu umuhumu wa wanadamu wote kuishi kwa pamoja  Gutteres amenukulu sehemu ya aya ya 13 ya Sura Hujurat katika Qur’ani Tukufu isemayo: “Enyi watu! Hakika Sisi tumekuumbeni kutokana na mwanamume na mwanamke. Na tumekujaalieni kuwa ni mataifa na makabila ili mjuane...”

/3474278

captcha