IQNA

Masomo ya waalimu wa Qur'ani yaanza tena Misri

19:43 - November 19, 2021
Habari ID: 3474579
TEHRAN (IQNA)- Vituo vya kuwafunza waalimu wa Qur'ani nchini Misri vinatazamiwa kuanza tena shughuli zao baada ya kufungwa kwa mwaka moja.

Wizara ya Wakfu Misri imetangaza kuwa, vituo hivyo vitaanza kazi Disemba 1 sambamba na vituo vyote vya utamaduni kote Misri.

Wizara hiyo imesema vituo hivyo vina nafasi muhimu katika kuwapa mafunzo waalimu ambao wanaeneza misimamo ya wastani ya Uislamu na kurekebisha itikadi potovu. Vituo hivyo pia vinastawisha utamaduni wa kuhifadhi Qur'ani.

Vituo vyote vya kufunzwa Qur'ani Misri, sawa na taasisi zingine za kidini, kielimu na kiutamaduni, zilifungwa mwaka jana ili kuzuia maambukizi ya COVID-19. Hadi sasa watu 347,000 wameambukizwa COVID-19 nchini Misri huku wengine 19,000 wakipoteza maisha kutokana na ugonjwa huo nchini humo.

4014419

captcha