IQNA

Benki ya Amana yazindua akaunti ya akiba ya Hija kwa Waislamu

22:27 - May 29, 2023
Habari ID: 3477068
TEHRAN (IQNA)- Benki ya Amana nchini Tanzania imezindua akaunti ya kuweka akiba ili kuwawezesha Waislamu kutekeleza ibada ya Hija.

Akaunti hiyo mpya ya akiba inalenga kurahisisha uwekaji akiba kwa ajili ya Waislamu wanaolenga

kutekeleza ibada ya Hija.

Akaunti hiyo mpya ya kuweka akiba, iliyopewa jina la ‘Hajj na Umrah’ inatarajiwa kuongeza idadi ya

Waislamu wanaohudhuria ibada ya Hija.

Ingawa Tanzania ina nafasi ya kupeleka Waislamu zaidi ya 20,000 kwa ajili ya Hija kila mwaka, lakini ni

1,000 tu, kwa wastani, wanaofanikiwa kutekeleza ibada hiyo kila mwaka.

Sasa, chini ya ufadhili mpya wa Benki ya Amana, idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka hadi angalau

Waislamu 3,000 ambao watarahisishwa kutekelea ibada ya Hija, ambayo ni safari ya kiroho na moja ya

nguzo tano za Uislamu.

Meneja wa Uzingatiaji wa Bidhaa na Sheria katika benki hiyo Bw Jamal Juma alisema hayo katika

uzinduzi uliofanyika katika Msikiti wa Jamiu-Zenjibar, Kiembesamaki.

Bw Juma alisema walichagua kuanzisha akaunti ya Hija na Umra ambayo inafaa zaidi watumishi wa

umma, na wastaafu.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Kibenki na Masoko wa Amana Bank, Dassu Mussa, alisema hapa kwamba

kwa mfumo huu mpya, Muislamu atalazimika kuweka akiba kwa miaka mitatu na benki itaongeza

asilimia 10 kwa wale ambao wanaweza kuhitaji kusafiri kabla ya pesa zinazohitajika kutumia/

Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo Sheikh Saleh Omar Kaab aliipongeza Benki hiyo kwa ufadhili huo mpya

huku akiwataka waumini wa Dini ya Kiislamu wenye sifa za safari hiyo kufanya hivyo kabla ya kuchelewa.

4143116

 

Kishikizo: hija ndogo
captcha