Akaunti hiyo mpya ya akiba inalenga kurahisisha uwekaji akiba kwa ajili ya Waislamu wanaolenga
kutekeleza ibada ya Hija.
Akaunti hiyo mpya ya kuweka akiba, iliyopewa jina la ‘Hajj na Umrah’ inatarajiwa kuongeza idadi ya
Waislamu wanaohudhuria ibada ya Hija.
Ingawa Tanzania ina nafasi ya kupeleka Waislamu zaidi ya 20,000 kwa ajili ya Hija kila mwaka, lakini ni
1,000 tu, kwa wastani, wanaofanikiwa kutekeleza ibada hiyo kila mwaka.
Sasa, chini ya ufadhili mpya wa Benki ya Amana, idadi hiyo inatarajiwa kuongezeka hadi angalau
Waislamu 3,000 ambao watarahisishwa kutekelea ibada ya Hija, ambayo ni safari ya kiroho na moja ya
nguzo tano za Uislamu.
Meneja wa Uzingatiaji wa Bidhaa na Sheria katika benki hiyo Bw Jamal Juma alisema hayo katika
uzinduzi uliofanyika katika Msikiti wa Jamiu-Zenjibar, Kiembesamaki.
Bw Juma alisema walichagua kuanzisha akaunti ya Hija na Umra ambayo inafaa zaidi watumishi wa
umma, na wastaafu.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Kibenki na Masoko wa Amana Bank, Dassu Mussa, alisema hapa kwamba
kwa mfumo huu mpya, Muislamu atalazimika kuweka akiba kwa miaka mitatu na benki itaongeza
asilimia 10 kwa wale ambao wanaweza kuhitaji kusafiri kabla ya pesa zinazohitajika kutumia/
Mgeni Rasmi katika uzinduzi huo Sheikh Saleh Omar Kaab aliipongeza Benki hiyo kwa ufadhili huo mpya
huku akiwataka waumini wa Dini ya Kiislamu wenye sifa za safari hiyo kufanya hivyo kabla ya kuchelewa.