IQNA

Kikao kuhusu uhusiano na utawala haramu wa Israel chaahirishwa nchini Morocco

19:04 - July 12, 2024
Habari ID: 3479112
IQNA - Mkutano uliopangwa na utawala katili wa Israel kuhusua uhusiano wa kawaida na Morocco umeakhirishwa katika nchi hiyo ya kasakzini mwa Afrika kutokana na hofu ya maandamano ya wananchi.

Israil iliripoti kucheleweshwa tukio hilo,  shirika la habari la Quds limeripoti

Kikao hicho kilipangwa kufanywa huko Casablanca kwa ushiriki wa wasomi wa Kiyahudi na. Kiislamu.

Spika  wa bunge la Morocco pia alipangwa kulihutubia kikao hicho.

Waandalizi wameahirisha tukio hilo kwa hofu kwamba watu waliokasirishwa na vita vya mauaji ya halaiki vya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza watafanya maandamano makubwa.

Mkutano huo umeakhirishwa mara mbili hapo awali, mara moja mwezi Mei,2024 na mara nyingine mwezi  Juni, 2024.  

Bado hakuna tarehe mpya iliyotangazwa ya mkutano huo.

Wananchi wa Morocco wamekuwa wakifanay maandamano makubwa makubwa tangu Desemba 10, 2020 kupinga hatua ya kuanzishwa uhusiano wa kawaida kati ya utawala wa kifalme nchini humo na utawala wa Kizayuni wa Israel katika makubaliano yaliyosimamiwa na utawala wa rais wa zamani wa Marekani Donald Trump.

Raia wa Morocco Wahimiza Kususia Biashara Zinazounga mkono utawala huo wa Israeli, Wataka Kukomeshwa kwa Kuhalalisha.
   
Nchi hiyo ya Afrika Kaskazini ilikuwa nchi ya nne ya Kiarabu kuhalalisha utawala mwaka huo. Nyingine zilikuwa Umoja wa Falme za Kiarabu, Bahrain na Sudan.

 

3489100

 

captcha