IQNA

Arbaeen 1446

Msikiti Mkubwa wa Kufa unawakaribisha Mazuwar wa Arbaeen

23:33 - August 24, 2024
Habari ID: 3479324
IQNA - Kila siku, makumi ya maelfu ya mazuwar au wafanyaziara wa Arbaeen hutembelea Msikiti Mkuu wa Kufa, ulioko karibu na Najaf, Iraq.

Msikiti Mkuu wa Kufa, ulioko takriban kilomita 12 kaskazini mwa Najaf, Iraq, ni moja ya misikiti muhimu zaidi katika ulimwengu wa Kiislamu.

Kwa Waislamu wa madhehebu ya Shia, unachukuliwa kuwa msikiti wa nne kwa umuhimu baada ya Masjid al-Haram jijini Makka,  Al-Masjid an-Nabawi jijini Madina na Masjid al-Aqsa jijini Al Quds.

Msikiti huo unaoaminika kuwa ulijengwa na Mtume Adam (AS), una historia ndefu na umekuwa ukitembelewa na Mitume na mawalii mbalimbali wakiwemo Mtume Muhammad (SAW), Imam Ali (AS), Imam Hassan (AS) na. Imam Hussein (AS).

Pia una makaburi ya watu mashuhuri kama Muslim ibn Aqeel, Hani ibn Urwa, na Al-Mukhtar, na umezungukwa na maeneo ya kihistoria, pamoja na nyumba ya Imam Ali (AS).

3489629

Kishikizo: Kufa arbaeen msikiti
captcha