IQNA

Ujue Msikiti wa Kufa na Mihrab ya Imam Ali (AS) + Video

8:45 - May 17, 2020
Habari ID: 3472773
TEHRAN (IQNA) - Msikiti wa Kufa ambao uko mjini Kufa Iraq ni katika ya misikiti mikubwa zaidi katika Ulimwengu wa Kiislamu na kwa Waislamu wa madhehebu ya Shia ni msikiti wa nne kwa utukufu baada ya Al-Masjid al-Haram, Al-Masjid an Nabawi (SAW) na Masjidul Aqsa.

Msikiti wa Kufa pia ni kati ya athari za kale na muhimu katika mji huo. Aidha katika msikiti huo kuna Mihrabu ya Imam Ali (AS) ambayo ni sehemu alipokuwa Imamu huyo mtukufu wakati alipopigwa dharba kwa upanga na ibn Muljam al-Muradi katika usiku wa 19 wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani katika mwaka wa 40 Hijria Qamaria.

  

3899368

captcha