TEHRAN (IQNA)-Katika kuonyesha mshikamano na uungaji mkono kwa Waislamu pamoja na familia za wahanga wa shambulio la kigaidi la Ijumaa iliyopita katika misikiti miwili ya Linwood na Al-Noor ya mji wa Christchurch nchini New Zealand, adhana imerushwa hewani kitaifa moja kwa moja katika televisheni na radio sambamba na misikiti yote ya nchi hiyo leo Ijumaa.
Habari ID: 3471885 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/22
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, katika ujumbe kwa munasaba wa kuanza mwaka mpya wa 1398 Hijiria Shamsia, ametuma salamu za pongezi za Nowuruz (Nairuzi) na pia salamu kwa munasaba Wilada ya Imam Ali AS kwa wananchi wa Iran na hasa familia za mashahidi na majeruhi wa vita na amelitakia taifa la Iran mwaka wenye furaha, saada, afya ya kimwili na mafanikio ya kimaada na kimaanawi na ameutaja mwaka mpya kuwa mwaka wa "kustawi uzalishaji".
Habari ID: 3471884 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/21
Rais Rouhani katika ujumbe wa Nowruz
TEHRAN (IQNA) - Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mapema Alhamisi ametuma ujumbe kwa kunasaba wa kuanza mwaka mpya wa 1398 Hijria Shamsiya na kusema mwaka 1397 ulikuwa mwaka wa mafanikio makubwa ya taifa la Iran katika nyuga mbali mbali na kuongeza kuwa, kwa yakini taifa la Iran litapata ushindi na litavuka matatizo yaliyopo.
Habari ID: 3471883 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/21
TEHRAN (IQNA)-Serikali ya Uingereza imetakiwa kuwapa Waislamu ulinzi kufuatia hujuma za Ijumaa iliyopita dhidi ya misikiti miwili nchini New Zealand.
Habari ID: 3471882 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/20
TEHRAN (IQNA)-Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadamu katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu ya Palestina Michael Lynk amesema upokonyaji wa maliasili za Wapalestina unaofanywa na utawala haramu wa Israel katika maeneo ya Palestina ni uporaji wa wazi.
Habari ID: 3471881 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/19
TEHRAN (IQNA) – Waziri Mkuu wa Malaysia Mahathir Mohammad amesema baadhi ya Waislamu hawana ufahamu sahihi wa Qur'ani na hivyo wanajihusisha na vitendo vilivyo kinyume cha mafundisho ya Uislamu.
Habari ID: 3471880 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/18
TEHRAN (IQNA) – Pale waumini walipokuwa wakimiminiwa risasi na gaidi wakati wa Sala ya Ijumaa msikitini, dereva wa texi, Abdul Kadir Ababora, alijificha chini ya rafu ambayo hutumika kuweka nakala za Qur'ani Tukufu huku akiomba Duaa kuwa apate fursa ya kubakia na mke na watoto wake.
Habari ID: 3471879 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/17
TEHRAN (IQNA)-Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani vikali hujuma za kigaidi zilizolenga misikiti miwili jana mjini Christchurch New Zealand na kupelekea Waislamu wasiopungua 49 kuuawa shahidi wakiwa katika Sala ya Ijumaa.
Habari ID: 3471878 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/16
TEHRAN (IQNA)- Waislamu wasiopungua 49, wakiwemo wanawake na watoto wadogo, wameuawa na wengine wasiopungua 48 wamejeruhiwa katika hujuma za kigaidi zilizofanywa dhidi ya misikiti miwili katika mji wa Christchurch nchini New Zealand wakati waumini wakiwa wamekusanyika kwa ajili ya Sala ya Ijumaa hii leo.
Habari ID: 3471877 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/15
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu asema:
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa kwamba adui mkuu wa taifa la Iran ni Marekani na kwamba kamwe taifa hili halitafanya kosa katika kumfahamu adui huyo.
Habari ID: 3471876 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/15
TEHRAN (IQNA)-Nchi 82 zinatazamiwa kuwa na wawakilishi katika Mashidani ya Kimataifa ya Qur'ani Tukufu nchini Iran mwaka huu.
Habari ID: 3471875 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/14
TEHRAN (IQNA)- Watoto wa shule moja ya chekechea ya Wakristo mjini Dusseldorf nchini Ujerumani wataanza kufunzwa Uislamu.
Habari ID: 3471872 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/12
TEHRAN (IQNA) – Waziri wa Elimu wa Iran Sayyid Mohammad Bathayi amesema takribani wanafunzi zaidi ya milioni mbili nchini Iran wanashiriki darsa za kuhifadhi Qur'ani.
Habari ID: 3471871 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/11
TEHRAN (IQNA)- Waislamu nchini Marekani wanabaguliwa zaidi ya wafuasi wa dini zingine zote nchini humo.
Habari ID: 3471870 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/10
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuhusu kuwepo uthabiti na amani nchini Myanmar. Aidha amesisitiza kuwa wakimbizi Waislamu wa jamii ya Rohingya warejeshwe haraka na kwa usalama katika makazi yao nchini Myanmar.
Habari ID: 3471869 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/09
Sayyid Hassan Nasrallah
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon Sayyid Hassan Nasrallah amesema kuwa, Marekani ilikuwa na njama kubwa tofauti kwa ajili ya kusambaratisha harakati hiyo mwaka 2006, lakini uimara wake umeweza kusambaratisha njama zote hizo.
Habari ID: 3471868 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/09
TEHRAN (IQNA)-Wananchi wa matabaka mbali mbali huko Algeria wameendeleza maandamani Ijumaa wakimtaka Rais Abdelaziz Bouteflika aondoke madarakani na asiwanie tena urais mwezi ujao wa Aprili.
Habari ID: 3471867 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/08
TEHRAN (IQNA)- Serikali ya Sudan imetangaza azma yake ya kuunga mkono madrassah za Qur'ani nchini humo ili kuhakikisha zinafanikiwa katika kustawisha elimu ya Qur'ani.
Habari ID: 3471864 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/06
TEHRAN (IQNA)- Sheikh Mkuu wa Al-Azhar wa Al Azhar amekosolewa na wanazuoni wenzake wa Kiislamu nchini Misri kwa kudai kuwa "ndoa ya wake wengi ni dhulma kwa wanawake na watoto".
Habari ID: 3471863 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/05
Mufti Mkuu wa Russia
TEHRAN (IQNA)- Waislamu wanatarajiwa kuongezeka na kufika asilimia 30 ya watu wote wa Russia ifikapo mwaka 2034 na hivyo kuna haja ya kujenga misikiti zaidi nchini humo.
Habari ID: 3471862 Tarehe ya kuchapishwa : 2019/03/05