Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu
TEHRAN (IQNA)-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, Palestina itaendelea kuwa taifa lenye nguvu na kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu, katika kipindi kisicho mbali sana taifa hilo litaweza kupata ushindi wa mwisho.
Habari ID: 3471792 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/31
TEHRAN (IQNA)- Mchezaji soka Msenegali ameashiria aya ya Qur'ani Tukufu kumtetea Kalidou Koulibaly Msenegali mwenzake ambaye ni difenda wa Timu ya Soka ya Napoli katika Ligia ya Italia ambaye amekumbana na matusi ya kibaguzi kutoka kwa mashabiki.
Habari ID: 3471790 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/29
TEHRAN (IQNA)- Wabunge katika muungano tawala nchini Ujerumani wamesema wanatafakari kuwashurutisha Waislamu kulipa ‘Ushuru wa Msikiti’ kama ambavyo Wakristo nchini humo wanatozwa ‘Ushuru wa Kanisa’.
Habari ID: 3471789 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/28
TEHRAN (IQNA)- Akademia ya Uislamu katika Sayansi na Jamii ya Chuo Kikuu cha Goethe nchini Ujerumani imetenga bajeti ya Euro milioni 2.7 katika mradi wa kufanya utafiti kuhusu Qur'ani Tukufu.
Habari ID: 3471788 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/27
TEHRAN (IQNA)- Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullahil Udhma Ali Khamenei leo asubuhi ameongoza Swala ya maiti ya marhumu ya Ayatullah Mahmoud Hashemi Shahroudi, aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Iran.
Habari ID: 3471787 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/26
TEHRAN (IQNA) Leo Disemba 25 inasadifiana na siku aliyozaliwa Nabii Isa Masiih- Amani Iwe Juu Yake (AS) kwa mujibu wa imani ya Wakristo waliowengi.
Habari ID: 3471786 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/25
Ayatullah Sayyid Mahmoud Hashemi Shahroudi, mwanazuoni maarufu wa Kiislamu nchini Iran ameaga dunia baada ya umri uliojaa baraka.
Habari ID: 3471785 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/25
TEHRAN (IQNA)- Waislamu katika mji wa Liverpool nchini Uingereza wanagawa misaada ya chakula kwa watu ambao hawana chakula katika kipindi cha Krismasi ambacho huandamana na baridi kali mjini humo.
Habari ID: 3471784 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/23
TEHRAN (IQNA)- Sheikhe Mkuu wa Chuo cha Kiislamu cha Al Azhar nchini Misri, Sheikh Ahmed al-Tayeb amemtumia salamu za Krismasi, Papa Francis, Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani.
Habari ID: 3471782 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/22
TEHRAN (IQNA)- Magaidi wakufurishaji wa kundi la Al Shabab wameua watu 16 katika hujuma ya kigaidi iliyojiri leo Jumamosi katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
Habari ID: 3471781 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/22
TEHRAN (IQNA)-Umoja wa Ulaya (EU) umetangaza kutenga bajeti ya Euro Milioni 10 kwa ajili ya utafiti wa kina kuhusu namna Qur'ani Tukufu imeathiri utamaduni wa Ulaya.
Habari ID: 3471780 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/21
TEHRAN (IQNA)-Askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel wameua watoto 54 Wapalestina mwaka huu wa 2018.
Habari ID: 3471779 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/20
TEHRAN (IQNA) Magaidi wakufurishaji wa kundi la ISIS (Daesh) wametekeleza mauaji mengine ya kutisha huko mashariki mwa Syria kwa kuua wafungwa mia saba karibu na eneo lililoko kwenye mpaka wa nchi hiyo na Iraq.
Habari ID: 3471778 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/20
TEHRAN (IQNA) – Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Saudi Arabia zimesaini Mapatano ya Maelewano (MOU) kuhusu kushiriki Wairani katika ibada ya Hija mwaka huu wa 1440 Hijria na 2019 Miladia.
Habari ID: 3471777 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/19
TEHRAN (IQNA) – Kituo kipya cha Qur'ani kimefunguliwa kwa ajili ya washichana wenye umri wa miaka 15 hadi 19 katika mji wa Fahad al Ahmad mkoa wa Al Ahmadi nchini Kuwait.
Habari ID: 3471776 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/18
TEHRAN (IQNA)- Tafsiri mpya ya Qur'ani inayojulikana kama 'Tafsiri ya Shams' imezinduliwa katika ofisi za Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa (IQNA) mjini Tehran.
Habari ID: 3471774 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/16
Dar al-Ifta ya Misri
TEHRAN (IQNA)- Huku Wakristo wakikaribia kusherehekea uzawa wa Nabii Isa AS (Yesu) katika siku ya Krisimasi na pia mwaka mpya Miladia, Taasisi ya Dar al-Ifta ya Misri imesema inajuzu au ni sawa kwa Waislamu kuwapongeza wasiokuwa Waislamu kwa munasaba wa siku kuu zao na kwamba hilo ni kwa mujibu wa mafundisho ya dini tukufu ya Kiislamu.
Habari ID: 3471773 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/16
TEHRAN (IQNA) – Washindi wa Mashindano ya 16 ya Kimataifa ya Qur'ani nchini Tunisia wametangazwa na kutunukiwa zawadi zao.
Habari ID: 3471772 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/15
TEHRAN (IQNA)- Bi. Linde McAvoy, alisilimu na kuukumbatia Uislamu maishani wiki chache baada ya kujiunga na Chuo cha Georgia Career Institute Conyers (GCI) katika jimbo la Georgia nchini Marekani mwezi Disemba 2017.
Habari ID: 3471771 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/15
TEHRAN (IQNA)- Waislamu nchini Nigeria wanakumbuka mauaji ya umati yaliyotekelezwa na jeshi la nchi hiyo dhidi ya wafuasi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria katika mji wa Zaria jimboni Kaduna.
Habari ID: 3471770 Tarehe ya kuchapishwa : 2018/12/14