
Hayo yamebainika katika taarifa iliyotolewa Jumamosi na Muungano wa Kitaifa wa Kuunga Mkono wa Kisheria ambao unaongozwa na Harakati ya Ikhanul Muslimin. Muungano huo umekuwa ukiandaa maandamano tokea Mursi alipopinduliwa. Katika taarifa, muungano huo umetoa wito kwa vyama vya kisiasa na wazalendo kuanzisha mazungumzo ya kina ili kutafuta njia za kuiondoa nchi hiyo katika mgogoro na kuhitimisha utawala wa kijeshi.
Misri ilitumbukia katika ghasia na machafuko tokea Julai 3 mwaka huu wakati jeshi lilipompindua rais Mursi na kumteua jaji wa Mahakama ya Katiba Adly Mahmoud Mansour kukaimu nafasi ya rais. Zaidi ya wafuasi 2,000 wa Mursi wameuawa katika kipindi cha miezi mitano iliyopita kufuatia hujuma ya vikosi vya usalama dhidi ya wanaopinga mapinduzi ya kijeshi.
1318246