Mwandishi wa Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa (IQNA) ameripoti kuwa, Imamu wa Msikiti wa Jamia wa Sanaa, Akram Ahmad al Ruqaihi amekadhibisha habari hiyo iliyochapishwa katika gazeti la al Umanaa. Amesema habari hiyo iliyochapishwa Jumatatu tarehe 17 Februari na kudai kuwa rais aliyeng'olewa madarakani wa Yemen Abdullah Saleh ametwaa nakala hiyo ya Qur'ani haina ukweli.
Imamu wa Msikiti wa Jamia wa Sanaa ameongeza kuwa, nakala hiyo ya Qur'ani Tukufu inahifadhiwa katika maktaba ya msikiti huo.
Awali gazeti la al Umanaa liliandika kuwa uongozi wa Msikiti wa Jamia wa Sanaa ulimpa kiongozi wa zamani wa Yemen nakala hiyo inayonasibishwa kwa Imam Ali bin Abi Twalib (as) inayojulikana kwa jina la Khatma ya Ali.
Uongozi wa Msikiti wa Jamia wa Sanaa umetangaza kuwa maktaba ya msikiti huo ambayo ina nakala muhimu na vitabu vilivyoandikwa kwa hati za mkono na vitabu nadra vya Kiislamu , mwezi Machi mwaka 2012 ilivamiwa na vitabu vyake kuibwa na watu wasiojulikana lakini nakala ya Qur'ani iliyoandikwa kwa hati za Imam Ali bin Abi Twalib (as) ilisalimika katika wizi huo. 1377069