IQNA

Qarii wa Iran asoma mbele ya mabalozi wa nchi za Kiislamu Uganda

21:50 - July 26, 2014
Habari ID: 1433643
Katika siku ya tano ya ‘Wiki ya Qur’ani kwa Himaya ya Iran’ , hafidh na qarii wa Qur’ani kutoka Iran wamesomba mbele ya mjumuiko wa mabalozi wa nchi za Kiislamu huko nchini Uganda.

Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA Afrika Mashariki, hafidh na qarii kutoka Iran pamoja na kundi la Qasida walishiriki katika hafla ambayo ilifanyika Kampala, mji mkuu wa Uganda na kuhudhuria pia na Musa Ali Naibu Waziri Mkuu wa Uganda, Naibu Waziri wa Afya, wabunge, mabalozi na wawakilishi wa nchi za Kiislamu kama vile Sudan, Saudi Arabia, Imarati, Libya na Misri.
Aidha hafla hiyo ilihudhuriwa pia na wahadhiri wa vyuo vikuu, mwakilishi wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt AS, mwakilishi wa Chuo Kikuu cha AL Mustafa AS Bw. Amir Hussein Nikbein, Balozi wa Iran nchini Uganda na Mwambata wa Utamaduni wa Iran katika jengo la Ubalozi wa Iran mjini Kampala.

1433490

Kishikizo: uganda qarii quran
captcha