IQNA

Ayatullah Araki: Nguvu za Waislamu ni katika umoja wao

15:28 - August 21, 2014
Habari ID: 1441626
Ayatullah Muhsin Araki, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kuzikurubisha Pamoja Madhehebu za Kiislamu amesema kuwa, miongoni mwa malengo muhimu ya risala ya Kiislamu na jukumu la Bwana Mtume SAW lilikuwa ni kuleta umoja baina ya watu

Ayatullah Araki amesisitiza kuwa, miongoni mwa majukumu muhimu ya mfumo wa Kiislamu ni kuleta umoja na mshikamano baina ya Waislamu. Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kuzikurubisha Pamoja Madhehebu za Kiislamu ameongeza kuwa, umoja ni msingi wa nguvu kwa jamii za Kiislamu. Ayatullah Muhsin Araki amebainisha kwamba, maadui wa Uislamu wanaulenga umoja wa jamii ya Kiislamu na wanafahamu kwamba, nguvu ya Waislamu iko katika umoja wao. Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kuzikurubisha Pamoja Madhehebu za Kiislamu ameeleza kuwa, ni kwa kuzingatia ukweli huo ndio maana maadui wamekuwa wakifanya njama za kuusambaratisha umma wa Kiislamu sambamba na kupanda mbegu za chuki na hasama baina ya makundi, madhehebu na kaumu mbalimbali katika ulimwengu wa Kiislamu.

1441061

Kishikizo: araki kiislamu umoja mtume
captcha