IQNA

Kiraa ya Nuaina, pambo la sherehe za kuhitimisha Mashindano ya Qurani ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu

14:44 - November 15, 2008
Habari ID: 1708415
Duru ya pili ya Mashindano ya Kimataifa ya Wanafunzi Waislamu wa Vyuo Vikuu kutoka nchi 40 duniani ilihitimishwa jana kwa kiraa ya msomaji mashuhuri wa Misri Ahmad Nuaina ambaye alikuwa mgeni makhsusi wa mashindano hayo.
Sherehe za kufunga mashindano hayo zilihudhuriwa na Meya wa jiji la Tehran, Muhammad Baqir Qalibaf, Mahdi Chamran Mkuu wa Baraza la Kiislamu la Mji wa Tehran, Rahim Khaki Mkuu wa Jumuiya ya Qur'ani ya Wanafunzi wa Vyuo Vikuu vya Iran, wabunge na shakhsia wengine wa kisiasa na kidini.
Mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani ya Wanafunzi Waislamu wa Vyuo Vikuu yalianza tarehe 10 mwezi huu wa Novemba katika ukumbi wa Kituo cha Kimataifa cha Milad na yalimalizika jioni ya jana kwa kutangazwa washindi wa mashindano hayo. 320044

captcha