Mkuu wa Kamati ya Mashindano hayo Fauzi al Anzi amesema kuwa mashindano ya Qurani ya Sharja yanafanyika katika sehemu mbili ya wanawake na wanaume na yanawashirikisha wawakilishi wa vituo 49 vya Qurani vya miji mbalimbali ya Umoja wa Falme za Kiarabu. Amesema kuwa washindani 130 wa kuhifadhi Qur’ani katika viwango na umri tofauti wanashiriki katika mashindano hayo yanayojumuisha kusoma na kuhifadhi Qur’ani Tukufu.
Mkuu wa Kamati ya Mashindano ya Qurani ya Sharja amesema, lengo la kutayarishwa mashindano hayo ni kuimarisha moyo wa ushindani kati ya washiriki, kuhamasisha usomaji na kuhifadhi Qur’ani Tukufu na kuelewa maneno ya Mwenyezi Mungu SW.
Amemalizia kwa kusema, washindi wa mashindano hayo watachaguliwa kwa ajili ya mashindano ya kimataifa ya Qur’ani Tukufu. 322706