IQNA – Kambi inayojumuisha mashindano matatu ya usomaji wa Qur’ani (Tilawa), warsha za ufundishaji, na hafla maalum ya watoto imepangwa kufanyika huko Mahibadhoo, mji wa kisiwani ulioko katikati mwa nchi ya Maldives.
Chuo cha Manfaa Academy kimejiandaa kuwa mwenyeji wa kambi hiyo ya Qur’ani.
Makamu wa Rais wa Manfaa Academy na meneja wa kambi hiyo, Mohamed Thaufeeq Ali, amesema kuwa shughuli hizo, zinazofanyika chini ya jina la “Kambi ya Qur’ani ya Manfaa” (Manfaa Quran Camp), ziko wazi kwa wakazi wa Mahibadhoo na visiwa vingine, na zitaendelea kuanzia tarehe 26 hadi 28 mwezi huu. Kwa mujibu wa Thaufeeq, wasomaji mahiri wa Qur’ani (Qari) watahudhuria ili kuongoza warsha, kutoa mihadhara, na kuwa majaji katika mashindano hayo wakati wa kambi hiyo.
“Programu nyingi zinazohusiana na Qur’ani zitaendelea katika kipindi hiki. Ndio maana inaitwa kambi, kwa sababu shughuli mbalimbali zimejumuishwa ndani yake. Wasomaji wengi maarufu wa Qur’ani kutoka Maldives watashiriki. Usomaji wao utasikika, na kutakuwa na warsha zitakazoongozwa na wasomaji hao,” alisema Thaufeeq.
Kambi hiyo itaendeshwa huko Mahibadhoo kwa msaada wa baraza la kisiwa hicho, Kituo cha Elimu cha Atoll (ADh. Atoll Education Centre), na mashirika kadhaa yasiyo ya kiserikali (NGOs).
Shughuli zitakazojumuishwa katika Kambi hiyo ni:
Kwa mujibu wa Thaufeeq, wakati ushiriki katika mashindano ya Qur’ani utafanyika kwanza kwa njia ya mtandao kupitia programu maalum (application), mchujo wa washiriki 30 bora utafanyika ana kwa ana huko Mahibadhoo.
Pia alibainisha kuwa zawadi nono zitatolewa kwa washindi katika mashindano yote matatu. Thaufeeq alieleza kuwa hafla ya watoto itajumuisha michezo inayolenga kuwajengea watoto mapenzi na ukaribu na Qur’ani. Hafla hiyo pia itatoa fursa kwa watoto kuuliza maswali na kupata maarifa kutoka kwa wasomaji wa Qur’ani watakaokuwepo.
Manfaa Academy inaendeshwa na Shirika la Manfaa, ambalo lilianzishwa na Ali Rameez.
3498664