IQNA

Kikao cha 'Mazungumzo ya Dini' kufanyika nchini Ufaransa

8:43 - November 23, 2008
Habari ID: 1711246
Ikiwa ni katika kuendeleza mfululizo wa vikao vyake kuhusiana na irfani katika dini za Kiyahudi, Kikristo na Kiislamu, Jumuiya ya Mazungumzi ya Dini ya Ufaransa imeandaa kikao maalumu kitakachojadili 'mazungumzo ya dini' hapo tarehe 26 Novemba katika ukumbi wa Pelloutier mjini Paris.
Waandaaji wa kikao hicho wamesema kuwa, lengo lake ni kuwakutanisha wafuasi wa dini hizi tatu kwa ajili ya kujadili maudhui ya 'kufahamu fikra za dini za mbinguni na kuishi pamoja kwa amani wafuasi wa Uyahudi, Ukristo na Uislamu.' Ni vyema kuashiria hapa kwamba Guy Levy na Julianne Unterberger, mkuu wa Jumuiya ya Kiutamaduni na Kijamii, Reims, watahutubia kikao hicho chini ya maudhui ya 'irfani katika Uyahudi.'
captcha