IQNA

Kongamano la ‘Mchango wa Wanawake Katika Ustawi wa Nchi za Kiislamu’ kufanyika Cairo

11:03 - November 23, 2008
Habari ID: 1711427
Kongamano la pili la ‘Mchango wa Wanawake Katika Ustawi’ ambalo linasimamiwa na Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC limepangwa kufanyika tarehe 24 na 25 za mwezi huu wa Novemba mjini Cairo, Misri.
Mwandishi wa IQNA ameripoti kuwa lengo la kongamano hilo ni kuchunguza sheria zinazohusiana na wanawake katika nchi za Kiislamu na kuimarisha nafasi yao katika nyanja za kijamii, kiutamaduni, kiuchumi na kisiasa.
Ajenda nyingine ya kongamano hilo ni kadhia ya kuwalinda wanawake kutokana na vitendo vya ukatili na ubaguzi na kutilia maanani suala la kuwaelimisha.
Kongamano la kwanza la Mchango wa Wanawake wa Kiislamu Katika Ustawi wa Nchi za Kiislamu lilifanyika Novemba 2006 katika mji wa Istanbul, Uturuki. 323974
captcha