Mwandishi wa IQNA ameripoti kuwa katika siku ya kwanza ya utekelezaji mpango huo, karibu wanawake 70 wa Kikristo wa Jumuiya ya Wanaharakati wa Kike wa Uholanzi walitembelea msikiti wa mji wa Utrecht.
Wanawake hao wa Kikatoliki walikutana na kufanya mazungumzo na maimamu wa misikiti na wanaharakati wa kike wa Kiislamu na kufafanuliwa misingi ya mafundisho ya dini ya Kiislamu.
Maimamu wa misikiti ya Uholanzi vilevile walijibu maswali ya wanawake wa Kikatoliki kuhusu ada na sheria za Kiislamu, adabu na kanuni za kuingia msikitini na sheria za udhu na adhana za kabla ya Swala. 324438