IQNA

Jordan yalaani kitendo cha Mayahudi cha kuingia Masjidul Aqsa

11:02 - December 06, 2008
Habari ID: 1716243
Waziri wa Habari na Mawasiliano wa Jordan amelaani kitendo cha Mayahudi 70 kuingia ndani ya msikiti mtakatifu wa al Aqsa wakisindikizwa na askari wa utawala ghasibu wa Israel.
Nasir Jauda amesema kuwa Jordan inalaani kitendo chochote kinachovunjia heshima maeneo matakatifu ya mji wa Quds. Amesema kuwa hatua hiyo itaamsha hasira za Waislamu na kwamba haiwezi kuhalalishwa kwa njia yoyote ile.
Waziri wa Habari wa Jordan ameutaka utawala wa Kizayuni wa Israel kuzuia hatua kama hizo na kuihimiza jamii ya kimataifa kufanya juhudi za kukabiliana na vitendo vya Israel vya kuvunjia heshima maeneo matakatifu ya Kiislamu. 330048
captcha