IQNA

Waislamu Australia wapinga wimbo wa taifa ulio dhidi ya Uislamu

9:32 - December 07, 2008
Habari ID: 1716549
Wakuu wa Chuo cha Kimataifa cha Kiislamu katika mji wa Brisbane Australia wamepinga kuimbwa wimbo wa tiafa ulio dhidi ya Uislamu katika shule hiyo.
Kwa mujibu wa gazeti la Kuwait la Al Qabas, wakuu wa shule hiyo katika mji wa Brisbane wamepinga kuimbwa wimbo huo ulio dhidi ya Uislamu wenye anwani ya "Ewe Australia, Endelea na Uadilifu". Mkuu wa zamani wa shule hiyo la Kiislamu ya Brisbane, Parveen Chand, amesema kuwa uongozi wa shule unasema, wimbo huo wa taifa unaenda kinyume na mafunzo pamoja na misingi ya dini ya Kiislamu na hivyo umepigwa marufuku shuleni hapo.
Wiki iliyopita, karibu Waustralia 300 wenye misimamo ya kufurutu mipaka walijumuika katika mji wa Gold Coast wa nchi hiyo na kupinga utolewaji leseni ya kujengwa shule mpya za Kiislamu nchini humo.
Waandamanaji wamedai kuwa kuasisiwa shule mpya za Kiislamu nchini humo kutaibua mgawanyika katika jamii ya nchi hiyo. 330507
captcha