IQNA

Kuhudhuria swala za jamaa kunaimarisha mshikamano wa Kiislamu

10:41 - December 08, 2008
Habari ID: 1717157
Utamaduni wa kusimamisha swala za jamaa unapaswa kuimarishwa na kuenezwa zaidi katika jamii kwa sababu unatayarisha uwanja wa mshikamano na umoja kati ya Waislamu.
Hayo yamesemwa na Mkuu wa Idara ya Ulinganiaji wa Kiislamu ya Miana nchini Iran Hujjatul Islam Ali Asghar Sayyadi ambaye ameongeza kuwa, ni wajibu wa wakuu wa idara mbalimbali kuhuisha swala za jamaa. Sheikh Ali Asghar amesema, wakuu wa idara mbalimbali wanatarajiwa kuwa mstari wa mbele wa swala za jamaa na kuwa kigezo cha kuigwa na wafanyakazi wengine.
Hujjatul Islam Ali Asghar Sayyadi ameashiria aya na hadithi zinazohimiza swala za jamaa na akasema: Swala za jamaa ni nembo ya umoja na mshikamano wa Kiislamu. 331025
captcha