Kikao cha kisomo cha dua ya Arafa kilitarajiwa kuanza saa nne na nusu asubuhi kwa wakati wa Zambia kwa kufunguliwa na kisomo cha Qur'ani Tukufu. Shughuli hiyo itaendelea hadi wakati wa swala ya Magharibi.
Lengo la shughuli hiyo ya kimaanawi na kiroho limetajwa kuwa ni kufafanua mafundisho aali ya Kiislamu kwa Waislamu wa Zambia.
Mkuu wa Kitengo cha Utamaduni cha Iran nchini Zambia Hujjatul Islam Asadi Muwahhid amesema kuwa katika shughuli hiyo Waislamu wa Zambia watajifunza maana na mafunzo ya tauhidi yaliyomo katika dua ra Arafa ambayo imepokelewa kutoka kwa Imam Hussein bin Ali (as) mjukuu wa Bwana Mtume Muhammad (saw).
Asadi amesema kuwa moja ya ajenda ya shughuli hiyo ni hotuba zitakazozungumzia maudhi ya 'Siku ya Arafa na nafasi ya siku hiyo muhimu katika Uislamu na Qur'ani" na "Falsafa ya Waislamu kuhudhuria katika uwanja wa Arafa huko Saudi Arabia."
331049