Kwa mujibu wa Arafat Ma'dhi, Mwenyekiti wa Kundi la wakazi wa Ulaya wanaotaka kukomeshwa mzingiro wa Gaza amesema: 'Wiki ya Gaza itafanyika mwezi Februari mwakani katika vyuo vikuu 100 barani Ulaya'. Amesema, kati ya harakati za wiki hiyo ni kuonyesha taswira za matatizo na masaibu ya watu wa Ukanda wa Gaza pamoja na jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel.
Mwanaharakati huyo wa Kiislamu amesema kuwa Umoja wa Ulaya haujachukua hatua zozote za maana kuhitimisha mzingiro wa Gaza. Amesema, nchi za Ulaya hazijaushinikiza utawala wa Kizayuni kusitisha hatua zake zilizo dhidi ya binadamu na za kidhalimu huko Palestina.
Arafat Ma'dhi amesema mzingiro wa Gaza ni kinyume cha sheria na kanuni zote za kimataifa. 332384