IQNA

Vitisho vya Marekani vitaunufaisha Uislamu

11:30 - December 13, 2008
Habari ID: 1718424
Ayatullah Qarebaghi ambaye ni Mjumbe wa Baraza la Wataalamu wa Kumchagua Kiongozi Mkuu wa Iran amesema kuwa Waislamu hawapaswi kuogopa nguvu za kijeshi za Marekani na kwamba vitisho vya nchi hiyo vinaunufaisha Uislamu.
Ayatullah Qarebaghi amesema kuwa vitisho au hata mashambulizi ya kijeshi ya Marekani dhidi ya nchi za Kiislamu hayawezi kuitokomeza dini hiyo na kwamba sera zao za kijeshi zinawazindua zaidi walimwengu na kuwafanya wawe macho kuhusu njama za nchi hiyo. Mwanazuoni huyo amesisitiza kuwa tatizo kubwa la wakati huo ni watu ambao wamevaa vazi la Uislamu na wanalitumia vazi hilo dhidi ya dini hiyo tukufu.
Ameashiria mchango wa maulama katika kueneza mafundisho ya Kiislamu na akatahadharisha juu ya njama za maadui wanaoeneza propaganda chafu dhidi ya madhehebu ya Ahlubaiti wa Mtume Muhammad (saw). 332483


captcha