Kwa mujibu wa gazeti la al Akhbar la Misri Abrus Baldisera mtaalamu wa maswala ya mashariki amesema kuwa nchi za Kiarabu hivi sasa zinakabiliwa na changamoto nyingi za kimatiafa kama vile kughusubiwa ardhi za Wapalestina na utawala wa haramu Israel ambao unatekeleza sera za kibaguzi.
Ameongeza kuwa, "nchi za Magharibi zina misimamo ya kindumakuwili kuhusiana na matatizo ya dunia jambo ambalo limeibua migogoro duniani. Wamagharibi wamewasilisha mpango wa mazungumzo ya kidini kama chombo tu cha kuendeleza malengo yao ya kibeberu".
Profesa Abrus Baldisera amesema kuwa, wataalamu wa masuala ya mashariki hawapaswi kuathiriwa na mitazamo na fikra za sera za Kimagharibi bali wanapaswa kuwa huru katika utafiti wao. 335767