Mkuu wa Benki ya Ustawi ya Kiislamu Ahmad Muhammad Ali amesema kuwa benki hiyo imetenga dola bilioni mbili kwa ajili ya kupambana na umaskini na kutekeleza miradi ya ujenzi katika nchi za Kiislamu katika mwaka 1430 Hijria.
Ahmad Muhammad Ali ameongeza kuwa, Mfuko wa Kustawisha Mshikamano wa Kiislamu pia utatoa mkopo wa dola milioni 357 kwa nchi wanachama wa Benki ya Ustawi ya Kiislamu kwa shabaha ya kupambana na umaskini katika ulimwengu wa Kiislamu. 338817