IQNA

Sherehe za Krismas katika nchi za Magharibi ni kinyume na ada za dini ya Kikristo

11:37 - December 28, 2008
Habari ID: 1723602
Imamu wa swala ya Ijumaa ya mji mtakatifu wa Najaf nchini Iraq amesema kuwa sherehe za Krismas katika nchi za Ulaya zinafanyika kinyume na ada za dini ya Kikristo na ni aina fulani ya kujitenga na Mwenyezi Mungu.
Sayyid Sadruddin al Qubanchi amewapongeza Wakristo wote duniani kwa mnasaba wa kuwadia mwaka mpya wa Miladia na akawahimiza wafuasi wa dini ya Nabii Issa Masih (amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake) kufaidika na mafundisho ya thamani ya mtukufu huyo na Bibi Maryam (as).
Sayyid al Qubanchi ameashiria kwamba, dini ya Kikristo haikubali ufuska na umaada unaotawala jamii za sasa za Magharibi na akasema: Wakristo wanaweza kurejea kwenye misingi ya Uislamu na mfumo wa Ahlubaiti wa Mtume kwa ajili ya kupata ufahamu sahihi wa mafundisho ya Issa Masiya (amani ya Mwenyezi Mungu iwe juu yake). Amewataka pia maaskofu wa Kikristo kubuni ratiba za kuwaongoza na kuwaelimisha Wakristo thamani halisi za dini hiyo wanapokuwa makanisani. 338682
captcha