IQNA

Chuo cha Kiislamu cha Gaza chalipuliwa na Wazayuni

10:02 - December 30, 2008
Habari ID: 1724769
Katika siku ya tatu ya mashambulio ya kinyama katika Ukanda wa Gaza, ndege za kijeshi za utawala haramu wa Israel zimeshambulia na kubomoa kabisa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Gaza.
Kwa mujibu wa televisheni ya al-Jazeera, ndege tano aina ya F16 za Israel jana zilifanya mashambulio ya kinyama katika maeneo ya makazi ya raia na kubomoa kabisa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Gaza. Mara tu baada ya kutekelezwa shambulio hilo la kinyama waokoaji walifika katika eneo hilo la kusini mwa Ukanda wa Gaza na kufanya operesheni za kuwaokoa wahanga wa shambulio hilo la Wazayuni. Hakuna habari zilizoweza kupatikana kwa haraka kuhusiana na idadi ya wahanga wa shambulio hilo. 340003
captcha