Gazeti la nchi hiyo la Peninsula limesema kuwa, washiriki 300 wa makundi mbalimbali ya Kiislamu kutoka nchi 75 za dunia watashiriki katika mkutano huo na kujadili changamoto na matatizo mbalimbali yanayoukabili umma wa Kiislamu katika zama hizi. Lengo la kuandaliwa mkutano huo ni kuandaliwa uwanja wa kupatikana harakati ya kimataifa ya Kiislamu kwa ajili ya kueneza amani, uadilifu na maelewano duniani.
Njia za kutatua matatizo ya Waislamu katika uliwemgu wa leo, uchunguzi wa misimamo ya kupindukia mipaka, kuimarishwa ushirikiano wa Waislamu na nchi za Magharibi na kujaribu kuwasilishwa sura halisi ya amani inayohubiriwa na Uislamu na Waislamu ni mambo yatakayojadiliwa katika mkutano huo. 345604