Kwa mujibu wa shirika la habari la Lematin, maonyesho hayo yanayofanyika kwa usimamizi wa Mfalme Mohammad wa Sita wa Morocco na mwenyekiti wa kamati ya Quds yanafanyika kwa lengo la kuonyesha nafasi ya Waislamu wa Morocco katika kulinda ardhi za Kiarabu na Kiislamu hasa Quds Tukufu katika zama za Watawala wa Kialawi.
Maonyesho ya "Morocco katika Quds" yanajumuisha picha na nyaraka za kipekee zinazoonyesha historia ya Waislamu wa Morocco huko Quds na ushawishi wao katika kuleta maelewano na mazungumzo ya kidini na vile vile nafasi ya sasa ya Morocco katika kutetea Wapalestina na Quds Tukufu katika nyanja mbalimbali.
Maonyesho hayo yamefanyika katika fremu ya kutangazwa mji wa Quds Tukufu kuwa mji mkuu wa utamaduni katika ulimwengu wa Kiarabu mwaka 2009. 353395