Kwa mujibu wa tovuti ya Ma'n, askari hao baada ya kuvamia kituo hicho, waliiba na kupora kila kitu cha thamani kilichokuwa humo na hatimaye kukifunga.
Kwa kufyatua risasi kiholela, askari hao wa Kizayuni walifukuza na kuwazuia Wapalestina wasikikaribie kituo hicho wala kufanya maandamano ya kulalamikia hatua hiyo ya kibaguzi katika kituo hicho cha Qur'ani.
Askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel vilevile walimtia nguvuni Sufyan Jadullah, mkuu wa kituo hicho na kukosea heshima nuskha za Qur'ani zilizokuwa katika kituo hicho. 359271