IQNA

Arbaeen ni fursa adhimu ya kueneza utamaduni wa Qur’ani ulimwenguni

17:37 - July 29, 2026
Habari ID: 3482558
IQNA – Mkuu wa Makao Makuu ya Kitaifa ya Arbaeen nchini Iran amesisitiza kuwa, matembezi ya kila mwaka ya kiroho ya Arbaeen yana uwezo mkubwa usio na kifani katika kukuza na kueneza utamaduni wa Qur’ani Tukufu miongoni mwa mamilioni ya mazuwaru (mahujaji).

Akizungumza na IQNA, Ndugu Ali Akbar Pourjamshidian alisema kuwa mkusanyiko huu mkubwa wa kijeshi na kiroho wa umma unaweza kuwa uwanja mkubwa zaidi wa kueneza utamaduni wa Qur’ani katika Ulimwengu wa Kiislamu.

“Ili kufikia lengo hili, shughuli za ki-Qur’ani lazima zinyanyuliwe kutoka kuwa programu za pembezoni na kuwa moja ya nguzo kuu za huduma za kitamaduni za Arbaeen.”

Naibu Waziri huyo wa Mambo ya Ndani alieleza kuwa shughuli za Qur’ani wakati wa ziara ya Arbaeen zimekuwa moja ya mihimili muhimu ya programu za tukio hili kubwa katika miaka ya hivi karibuni. Mtazamo huu, mbali na kuandaa vikao vya usomaji wa Qur’ani (tilaawah), unajumuisha pia vikao vya kutafakari aya za Mwenyezi Mungu, mashindano, na programu maalum kwa ajili ya watoto na vijana, kwa lengo la kubadilisha dhana za Qur’ani kuwa mtindo wa maisha.

Pourjamshidian alikariri umuhimu wa kuendeleza shughuli za Qur’ani katika mkusanyiko huu mkubwa wa kijeshi-kiutamaduni wa wananchi, akiashiria uwezo wa kipekee wa Arbaeen katika kuimarisha maadili ya Kiislamu.

Akigusia maendeleo ya kitamaduni ya miaka ya hivi karibuni, alisema kuwa Shirika la Maendeleo ya Kiislamu la Iran limechukua hatua za thamani na zenye athari kubwa nchini kwa kulenga hasa uwanja wa Qur’ani na mafundisho yake.

“Mtazamo huu umefanya shughuli za Qur’ani kuacha kuwa programu za msimu tu na badala yake kuwa sehemu ya mkondo wa kitamaduni na maisha ya kila siku ya jamii.”

Alieleza kuwa leo hii, umakini mkubwa unaelekezwa katika kuhifadhi Qur’ani, kuelewa maana ya aya za Mwenyezi Mungu, na kutumia mafundisho hayo katika maisha ya mtu binafsi na ya kijamii, jambo ambalo linafungua njia ya kujenga jamii yenye misingi ya maadili ya Qur’ani.

Pia aliashiria utekelezwaji wa mpango wa kitaifa wa “Maisha na Aya za Qur’ani” , akiuelezea kuwa ni moja ya programu zilizofanikiwa zaidi za Qur’ani katika miaka ya hivi karibuni. Huu ni mpango unaojaribu kupeleka dhana za Qur’ani mbali zaidi ya elimu ya darasani na kuziingiza katika maisha ya kila siku ya wananchi.

Akisisitiza kuwa athari chanya za mpango huo zinaonekana wazi katika sehemu mbalimbali za nchi, alisema kuwa Wizara ya Mambo ya Ndani, kwa ushirikiano na Shirika la Maendeleo ya Kiislamu, ilitekeleza mpango huu kwa majaribio katika baadhi ya mikoa na taasisi za kiserikali, na matokeo yalionyesha kuwa kuna utayari mkubwa wa kuendeleza utamaduni wa Qur’ani miongoni mwa watumishi wa umma.

Aliendelea kusema kuwa ikiwa Qur’ani itakuwa muhili wa programu za kitamaduni za nchi, changamoto na madhara mengi ya kijamii, kitamaduni, na kimaadili yatapungua.

“Kulingana na hili, Wizara ya Mambo ya Ndani iko tayari kutoa uwezo wake mkubwa kwa ajili ya kuendeleza programu za Qur’ani, hasa katika matukio adhimu kama vile Arbaeen ya Imam Hussein (AS).”

3498451

captcha