IQNA

CAIR yampongeza Obama kwa kutumia hadithi ya Mtume katika hotuba yake

10:41 - February 07, 2009
Habari ID: 1741065
Baraza la Uhusiano wa Uislamu na Marekani (CAIR) limekaribisha hatua ya Rais Barack Obama wa Marekani ya kutumia hadithi ya Mtume Muhammad (saw) katika hotuba yake kwenye sherehe ya kitaifa mjini Washington.
Mkurugenzi wa masuala ya kisheria wa CAIR amekaribisha hotuba ya Obama kuhusu suala la kueneza amani na uvumilivu kote duniani akitegemea maneno yenye thamani ya Mtume Muhammad (saw) katika uwanja huo na akasisitiza kwamba: CAIR inatarajia kuona wafuasi wa dini zote wakiheshimiwa duniani hususan Marekani katika siku zijazo na kuondolewa nyufa zilizopo katika medani hiyo.
Alkhamisi iliyopita Rais Barack Obama wa Marekani alihutubia kikao cha wawakilishi wa bunge, shakhsia wa kidini na wawakilishi nchi kadhaa duniani na pamoja na kuzungumzia vipengee vya Taurati na Injili, alinukuu pia hadithi ya Mtume Muhammad (saw) akisema: Katika Uislamu kuna hadithi inayosema: Muislamu wa kweli ni yule anayewatakia wenzake kile anachokipenda yeye.
Obama amesisitiza kwamba, lengo la dini zote ni kuwalingania wanadamu amani, upendo, maisha ya suluhu na kuheshimiana. 360183

captcha